Hatimaye Uingereza kuirejesha Chagos kwa Mauritius
2 Aprili 2025Matangazo
Taarifa iliyotolewa jana na serikali ya Uingereza imesema baada ya mkataba huo kukamilika, utawasilishwa kwenye bunge la nchi hiyo kwa majadiliano.
Tayari, London imeshawasiliana na utawala wa Rais Donald Trump wa Marekani, ambao umetowa baraka zake kwa hatua hiyo.
Uingereza, ambayo ni mkoloni wa zamani wa Mauritius, ilikitwaa kisiwa hicho kwa nguvu wakati ilipotowa uhuru kwa taifa hilo la mashariki mwa Afrika.
Hata hivyo, Mauritius ilishinda kesi kwenye Mahakama ya Haki ya Kimataifa, ICJ, iliyoamuwa kuwa Chagos ni sehemu ya mamlaka ya Mauritius.