Hatimaye Michuano ya CHAN kuanza kutimua vumbi Jumamosi
1 Agosti 2025Matangazo
Ukarabati huo ulichelewa kwa muda na kusogeza mbele muda wa michuano hiyo ambayo awali ilipangwa kuanza mwezi Februari. Na sasa kinyang'anyiro hiki kilichosubiriwa kwa hamu kitaanza siku ya Jumamosi (Agosti 2, 2025).
Shirikisho la Soka barani Afrika CAF lililazimika kuisogeza michuano hiyo mbele ili kutoa muda wa kukamilishwa kwa viwanja vitano ambavyo vingetumika kwenye michuano hiyo.
Ni wakati wa kihistoria kwa Kenya, Tanzania, na Uganda, wanaoandaa michuano hiyo kwa pamoja kufuatia ombi la miaka miwili iliyopita na kupelekea michuano hiyo ya CAF kufanyika kwa mara ya kwanza katika ukanda huo tangu 1976 na ya kwanza kuandaliwa na nchi tatu kwa pamoja.