JangaKimataifa
Hatari ya Tsunami katika pwani ya Pasifiki yapungua maradufu
30 Julai 2025Matangazo
Tetemeko hilo lenye ukubwa wa 8.8 katika kipimo cha Richter lilipiga huko Kamchatka katika pwani ya mashariki mwa Urusi mapema Jumatano.
Awali, mataifa ya Japan, China, Marekani, Ufilipino, Mexico na Ecuador, yalitangaza hali ya tahadhari na kuwataka wakazi wa maeneo ya pwani kujiandaa na uwezekano wa kutokea janga la Tsunami ambalo lingehatarisha maisha ya mamilioni ya watu.
Lakini saa chache baada ya tetemeko hilo kutikisa Mashariki ya mbali ya Urusi, hakujaripotiwa taarifa za uharibifu mkubwa, huku tahadhari ya Tsunami ikionekana kupungua maradufu katika maeneo mengi yaliyokuwa hatarini.