Hamas yatoa wito dhidi ya mpango wa Trump kwa Gaza
31 Machi 2025Matangazo
Katika taarifa, Abu Zuhri amesema kuwa katika kukabiliana na mpango huo aliouita mbaya na unaochanganya mauaji na njaa, mtu yeyote anayeweza kubeba silaha, popote duniani, lazima achukue hatua.
Israel yapendekeza mpango mpya wa kuachiwa mateka
Wito huo wa Abu Zuhri unatolewa siku moja baada ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kuamua kuwaacha viongozi wa Hamas kuondoka Gaza, lakini akalitaka kundi hilo la wanamgambo wa Palestina kusalimisha silaha zao katika hatua za mwisho za vita katika ukanda huo.
Hamas imeeleza nia ya kuachia utawala wa Gaza, lakini imeonya kuwa silaha zake ni eneo lisilopaswa kufikiwa.