MigogoroIsrael
Hamas yamwachia mwanajeshi wa Israel
30 Januari 2025Matangazo
Mikanda ya video imeonesha wanamgambo waliofunika nyuso zao wakimwachia huru mwanajeshi wa Israel, Agam Berger na kisha kumkabidhi kwa wafanyakazi wa Shirika la Msalaba Mwekundu katia tukio lililofanyika kwenye kambi ya wakimbizi ya Jabalia, kaskazini mwa Gaza.
Kwa jumla, Waisraeli watatu pamoja na raia watano wa Thailand wataachiwa huru leo tangu walipotekwa nyara Oktoba 7, 2023 wakati wa mashambulizi ya kundi la Hamas ndani ya ardhi ya Israel.
Katika awamu hii ya sasa ambayo ni ya tatu tangu kutiwa saini makubaliano ya kusitisha vita Ukanda wa Gaza, wafungwa 110 wa Kipalestina nao wataachiwa kutoka jela za Israel wanakozuiliwa.