Hamas: Israel inatumia "njaa kama silaha ya vita" huko Gaza
17 Aprili 2025Israel ilisema siku ya Jumatano kuwa hakuna msaada wowote wa kibinadamu utakaoruhusiwa kuingia katika ardhi ya Palestina huku waziri wake wa ulinzi Israel Katz akidai, hiyo ni mojawapo ya njia kuu za kuishinikiza Hamas iwaachie mateka, huku ikilituhumu kundi hilo la wanamgambo kwa kuichukua misaada hiyo ili liuendeleze utawala wake.
Hayo yakiarifiwa, shirika la ulinzi wa kiraia huko Gaza limesema leo kwamba wimbi la mashambulizi ya anga ya Israel kwenye kambi nyingi za Wapalestina waliokimbia makazi yao limesababisha vifo vya watu 25.
Soma pia: Ripoti mpya inaonesha hatari kubwa ya njaa inaigubika Gaza
Msemaji wa shirika hilo Mahmud Bassal amesema mashambulizi ya usiku wa kuamkia leo yalilenga mahema kadhaa katika eneo la Al-Mawasi katika mji wa kusini wa Khan Yunis, na katika mji wa kaskazini wa Beit Lahia.