Sweida sasa ni tulivu baada ya mapigano makali ya kidini
20 Julai 2025Shirika hilo likinukuu taarifa kutoka wizara ya ndani nchini Syria, limesema wapiganaji wote wameondolewa mjini Sweida na mapigano yamemalizika. Hata hivyo shirika la uangalizi wa haki za binaadamu la Syria limesema kuna utulivu lakini sio wa uhakika.
Waziri wa habari wa Syria Hamza Al-Mostafa, amesema bado wanafuatilia hali ilivyo mjini humo...
"Muda unaotarajiwa wa awamu ya kwanza, ambao unahusisha kusitisha mapigano, ni saa 48. Kwa kuzingatia hilo, hali itatathminiwa ili kuendelea na awamu ya pili. Kwa hiyo, haiwezekani kujua muda maalum katika hatua hii."
Syria yatangaza usitishwaji mapigano katika jimbo la Sweida
Mapigano mjini humo yaliyoanza wiki moja iliyopita yalisababisha mauaji ya maelfu ya watu, hali ngumu ya kibinaadamu huku maelfu ya watu wakiuhama mji huo. Awali waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani Marco Rubio alitoa wito wa mapigano kukomeshwa mara moja.
Hali bado inaripotiwa kuwa tete chini ya rais mpya wa Syria Ahmed al-Sharaa, alieingia madarakani baada ya kumuondoa rais wa muda mrefu Bashar Al Assad miezi sita iliyopita. Lakini wakati utawala wake ukiahidi kurejesha uthabiti nchini humo bado kunashuhudiwa mapigano ya kikabila, vurugu za wanamgambo na mashambulizi ya kigaidi.