MigogoroUlaya
Gwaride la jeshi la wanamaji wa Urusi laahirishwa ghafla
27 Julai 2025Matangazo
Maonyesho hayo ya meli za kivita na uwezo wa jeshi hilo yalitakiwa kufanyika leo katika mji wa St Petersburg. Siku hiyo ya jeshi la Wanamaji wa Urusi iliyozinduliwa kwa mara ya kwanza mnamo mwaka 2017 na rais wa Vladimir Putin, hufanyika Jumapili ya mwisho ya mwezi Julai kila mwaka na huwaenzi mabaharia wa nchi hiyo.
Hayo yanaripotiwa wakati Urusi na Ukraine zimeendelea kushambuliana vikali kwa makombora na droni na kusababisha vifo kila upande. Moscow imesema imedungua usiku wa kuamkia Jumapili droni karibu 100 zilizorushwa na Ukraine.