Brice Oligui Nguema aapishwa kuiongoza Gabon
3 Mei 2025Matangazo
Nguema aliongoza mapinduzi ya kijeshi dhidi ya utawala wa familia ya Bongo uliodumu kwa miaka 55. Miongoni mwao ni Rais wa Gambia Adama Barrow, Bassirou Diomaye Faye wa Senegal, Ismail Omar Guelle wa Djibouti na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Felix Tshisekedi.
Soma zaidi: Nguema aapa kurejesha hadhi ya raia wa Gabon
Rais huyo mteule wa Gabon, mwenye miaka 50 anakabiliwa na changamoto kubwa katika nchi hiyo zikiwemo miundombinu chakavu ya umeme inayosababisha kukatika kwa umeme mara kwa mara, ukosefu wa ajira kwa vijana, bila kusahau deni kubwa la taifa.