Merz ashindwa kupitishwa na Bunge kuwa Kansela wa Ujerumani
6 Mei 2025Matangazo
Merz, alitarajiwa kushinda kura hiyo na alihitaji wingi wa kura 316 kati ya 630 zilizopigwa kwa siri lakini hatimaye alipata kura 310 pekee. Kwa sasa vyama hivyo vya siasa vitajipanga upya ili kujadili hatua inayofuata.
Soma pia: Merz ashindwa kuwa kansela duru ya kwanza ya kura bungeni
Serikali ya mseto ilitarajiwa kuongozwa na CDU/CSU pamoja na chama cha siasa za wastani za mrengo wa kushoto cha SPD, ambacho ni cha kansela anayeondoka mamlakani, Olaf Scholz aliyeagwa rasmi hapo jana.