Fletcher: Sheria sawa zinatumika kwa Israel kama dola zote
17 Julai 2025Mratibu Mkuu wa misaada ya dharura wa Umoja wa Mataifa, Tom Fletcher amelihimiza Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kutathmini ikiwa Israel inatimiza majukumu na ahadi yake katika Ukanda wa Gaza, huku akionya kwamba hali ya kibinadamu imekuwa janga.
Akizungumza jana Jumatano mjini New York, Fletcher amesema Israel ina wajibu wa kuhakikisha watu wa Gaza wana chakula na dawa, lakini hilo halifanyiki. Badala yake raia wanakabiliwa na hatari ya kifo kwa kupigwa risasi, kujeruhiwa na kulazimishwa kuyahama makazi yao na kudhalilishwa utu wao.
Wakati hayo yakiarifiwa, shambulizi dhidi ya kanisa pekee la Katoliki Gaza limewajeruhi watu kadhaa, akiwemo padri mmoja na kusababisha uharibifu kwa jengo la nyumba hiyo ya ibada. Jeshi la Israel limesema linachunguza tukio hilo.