SiasaAsia
FBI yaituhumu Korea Kaskazini kwa wizi wa dola bilioni 1.5
27 Februari 2025Matangazo
Tangazo kwa umma lililotolewa na FBI siku ya Jumatano (Februari 26) lilisema wahusika wa kundi hilo wanafanya kazi kwa kasi kubwa na tayari wamefanikiwa kuzibadilisha mali walizoiba kuwa safaru za mtandaoni na huku mali nyengine wakizisambaza maeneo mbalimbali ulimwenguni.
FBI ilisema inatazamia kuwa mali hizo zitatakatishwa kwa njia haramu na baadaye kugeuzwa kuwa fedha rasmi.
Soma zaidi:
Kampuni ya sarafu za mtandaoni ya ByBit ilisema siku ya Ijumaa kwamba mshambulizi wa mtandaoni alifanikiwa kutwaa udhibiti wa akaunti yake na kuzihamishia mali zake kwenye anwani zisizotambulika.
Kampuni ya ubadilishaji fedha inahudumia zaidi ya watumiaji milioni 60 ulimwenguni.