Europol yasema mtandao wa udukuzi wasambaratishwa
16 Julai 2025Matangazo
Katika taarifa, Europol imesema kuwa hatua hiyo ilisababisha kukatika kwa miundombinu ya mashambulizi inayojumuisha zaidi ya mifumo mia moja ya kompyuta duniani kote, wakati sehemu kubwa ya miundombinu ya seva kuu ya kundi hilo ikikatizwa .
Mifumo ya kompyuta Ujerumani yadukuliwa
Mamlaka imetoa waranti saba za kimataifa za kukamatwa kwa washukiwa, zikiwemo sita kwa washukiwa walioko nchini Urusi.
Taarifa hiyo imeendelea kusema kuwa watu wawili kati ya washukiwa hao wanaaminika kuwa waandaaji wakuu wa shughuli za kundi hilo.
Masharika hayo yamesema kuwa shughuli za mtandao huo zilitatizwa kufuatiauvamizi katika nchi 12 kati ya Julai 14 na 17.